300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Oct 4, 2013

Tagged under: ,

HotNewz| Rwanda yashangazwa na hatua ya Marekani.


Kigali, Rwanda
Jeshi la Rwanda limeiokosoa Marekani baada ya kuiwekea vikwazo kwa madai kwamba limekuwa likiwasaidia wapiganaji wa Kundi la M23.
Taarifa zilisema kuwa Marekani ilichukua uamuzi huo baada ya kulituhumu Jeshi la Rwanda kwamba liliwasaidia wapiganaji wa M23 waliopo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuwatumikisha watoto jeshini.
Msemaji wa Jeshi la Rwanda, Joseph Nzabamwita alisema kuwa tuhuma hizo za Washington hazina ukweli na wala hazina ushahidi wowote.
Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilitangaza kuwa nchi hiyo ilisimamisha misaada ya kifedha na kijeshi kwa nchi hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2014.
Wakati huohuo, ujumbe wa wataalamu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ulielekea katika eneo la Ukanda wa Maziwa Makuu ya Afrika kwa shabaha ya kutoa msukumo wa usalama na amani katika eneo hilo.
Taarifa ya Umoja wa Mataifa ilieleza kuwa, ujumbe huo utakutana na marais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda, Uganda na Waziri Mkuu wa Ethiopia.
Umoja wa Mataifa unaituhumu Rwanda kwa kuwaunga mkono M23 katika harakati zao dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo madai ambayo Rwanda imekana.

Kundi  la M23 lilianzishwa na waliokuwa waasi wa Kitutsi waliojiunga na Jeshi la DRC chini ya mkataba wa amani wa mwaka 2009
Mwaka 2012 mwezi Aprili waasi hao wa M23 waliwageuka waliokuwa wanajeshi wenza na kuanza uasi Mashariki mwa nchi ambako kuna utajiri mkubwa wa madini.

SOURCE:
Mwananchi

0 your comments:

Post a Comment