300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Oct 1, 2013

Tagged under: ,

Michezo| Akina Boateng walivyo na undugu wa mashaka



KIUNGO wa Schalke 04, Kevin-Prince Boateng na mdogo wake, Jerome Boateng anayekipiga Bayern Munich wanachekesha sana. Ni ndugu wa baba mmoja, lakini wanatoka matumbo tofauti.
Kama hiyo haitoshi, makuzi yao ya mahangaiko jijini Berlin yamewafanya wawe na bifu za kitoto pia.
Amnyima tiketi mdogo wake
Wiki iliyopita, Bayern Munich ilisafiri mpaka Schalke kukipiga na Schalke 04 katika pambano la Ligi Kuu Ujerumani. Pambano hilo lilipigwa katika Uwanja wa Gelsenkirchen.
Kabla ya mechi, Jerome alimuomba tiketi ya bure kaka yake kwa ajili ya kumpatia rafiki yake au mpenzi wake. Hata hivyo saa chache kabla ya mechi, Kevin alimtumia mdogo wake ujumbe katika simu uliosomeka: “Siwezi kukupatia tiketi yoyote. Samahani.”

Jerome alifichua siri hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari huku akikiri kwamba ni wazi kwamba kaka yake alikuwa amemnyima tiketi. Si tiketi tu, Kevin ana chumba chake maalumu cha kutazamia mechi uwanjani Gelsenkirchen katika eneo la watu maalumu, lakini alikuwa ameamua tu kumfanyia roho mbaya mdogo wake.
Wakati wa mapumziko wa pambano hilo, wawili hao walikumbatiana kwa furaha na kubadilishana jezi, huku wakiongea maneno mawili matatu.
Baba yao ataka wakasirikiane
Baba yao anayejulikana kwa jina la Prince Boateng aliondoka nchini Ghana mwaka 1981 kwenda Ujerumani kwa ajili ya kusoma masomo ya Utawala.
Hata hivyo masomo yalimshinda na badala yake akaingia katika kazi ya muziki akiwa DJ na vile vile akiwa mhudumu wa baa.
Kevin-Prince alikuwa na umri wa miaka miwili wakati baba huyo alipoiacha familia nyumbani na kusababisha mama yake wa Kijerumani atumie muda mwingi kuwalea yeye na mdogo wake, Jerome ingawa mama wa Jerome ni mwingine.

SOURCE 
Mwanasport

0 your comments:

Post a Comment