300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Apr 15, 2016

Tagged under: , ,

Kutoka Majuu| Jimbo la Arizona Marekani Kuhalalisha Bangi ifikapo Novemba.



Jimbo la Arizona nchini marekani limeanzisha mchakato wa kuahalalisha Bangi iwe kilevi kama vilevi vingine ikiwemo Pombe.
Mchakato huo ambao ulitangazwa jumanne ya April 12 mwaka huu,kwa sasa upo  kwenye uchukuaji wa Saini za wakazi wapatao  201,158.

Kwa mujibu wa mtandao wa Kampeini hiyo  unatarajia kukusanya zaidi ya Saini  201,158  ili kuruhusu zoezi kufanikiwa kwa kuwa baadhi ya watakaoweka Saini hawatojitokeza kupiga kura ya kuipitisha sheria hiyo ifikapo mwezi Novemba mwaka huu ambapo nusu ya kura zitakazopendekeza Bangi iwe Kilevi sawa na vilevi vingine itaruhusiwa kisheria kutumiwa na watu walio zaidi ya umri wa miaka 18.

Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi kufikia Juni mwaka huu jumla ya Saini 150,642 zinahitajika kutoka kwa watu waliosajiliwa kushiriki chaguzi mbalimbali katika jimbo la Arizona ili kuona ulinganifu wa zoezi la upigwaji kura Mwezi Novemba mwaka huu.
Kampeni hiyo ya kuihalalisha Bangi iwe kilevi halali kama Vilevi vingine unaratibiwa na mpango maalum ambapo kwa sheria za utumiaji Madawa ya kulevya katika jimbo hilo kodi asilimia 15 inatoka katika upande wa Bangi japo haitumiki kihalali kwa matumizi ya kilevi lakini kiwango kinachopatikana kutokana na kodi hiyo hupelekewa katika shughuli za kijamii ikiwemo shule za serikali katika jimbo hilo.

Kwa mujibu wa Waratibu wa Kampeni ya kuruhusu Bangi iwe sawa na Vilevi vingine wanadai huenda kampeni hiyo isifanikiwe kulinagana na uzito wa sheria za Marekani unaobana Matumizi ya Bangi kihalali japo yanatumiwa na Wamarekani.

Kusoma zaidi BOFYA HAPA 

0 your comments:

Post a Comment