300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Feb 18, 2013

Tagged under: ,

News & Social | Madai ya njama ya wizi wa kura uchaguzi ujao Kenya

kushoto ni mgombea kwa tiketi ya chama cha ODM(Orange Democratic Movement) Raila Odinga,kulia ni Uhuru Kenyatta toka chama cha Nationa Alliance Party(NAT)
          Serikali ya Kenya imekanusha madai kuwa kuna njama ya wizi wa kura katika uchaguzi mkuu ujao mwezi Machi 4 kwa niaba ya Muungano wa Jubilee wake Uhuru Kenyatta.Msemaji wa serikali Muthi Kariuki alisema kuwa madai yaliyotolewa na muungano wa CORD wake waziri mkuu Raila Odinga hayana msingi na kuna hofu kuwa huenda madai hayo yakachochea hali ya wasiwasi na taharuki miongoni mwa wafuasi wa pande hizo mbili.
''Ni lazima watu wafahamu kuwa mkuu wa idara ya ujasusi Julius Karangi, anayesemekana kufanya mkutano kuhusu njama ya wizi wa kura, wakati huo alikuwa nchini Uganda kwa hivyo inawezekanaje alikuwa na mkutano? alihoji msemaji wa serikali Muthui Kariuki.
Aliutaka Muungano wa Cord kutafuta sera za kuwauzia wakenya ili waweze kuwachagua badala ya kueneza propaganda na kutishia usalama wa nchi
       Bwana Muriuki alisema kuwa mkuu wa utumishi wa Umma, Francis Kimemia alitoa onyo kwa wafanyakazi wa umma kuwaonya wafanyakazi wa umma dhidi ya kujihusisha na kampeini au maswala ya siasa.Madai ya CORD yamekuja wakati pande zote mbili zinarushiana madai ya njama ya wizi wa kura. Wiki iliyopita Jubilee au upande wa Uhuru Kenyatta ulidai kuwa pande CORD wana njama ya kuwalewesha wapiga kura wao usiku mkesha wa uchaguzi.

0 your comments:

Post a Comment