300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Feb 18, 2013

Tagged under: ,

Social & News | Kundi la Wapiganaji(Ansaru)limedaiwa kuwateka nyara wafanyakazi nchini Nigeria

        Kundi la wapiganaji la Ansaru, limedai liliwateka nyara wafanyakazi saba wa kigeni na kumuua mlinzi wakati wa tukio hilo.Wafanyakazi kutoka Italia, Ufilipino, Uingereza, Ugiriki na Lebanon yasemekana ni kati ya wale waliotekwa nyara katika jimbo la Bauchi Kaskazini mwa Nigeria.Wafanyakazi hao walikuwa kazini katika kiwanda kimoja wakati wapiganaji hao walipowateka nyara siku ya Jumapili.
      Mapema leo, polisi nchini humo walianzisha msako dhidi ya watu waliowateka nyara wafanyakazi hao.
Mlinzi katika kampuni hiyo ya ujenzi, Septraco, inayomilikiwa na watu wenye asili ya Lebanon, alipigwa risasi na kuuwawa kwenye ua la kampuni hiyo.Septraco inapanua barabara moja kuu katika jimbo la Bauchi. Awali, kituo cha polisi katika mji wa Jama'are kilishambuliwa na magari mawili kulipuliwa.
        Mapema mwezi huu, watoa chanjo za polio tisa walipigwa risasi na kuuwawa katika zahanati mbili hukuhuko kaskazini mwa Nigeria.Kudni la Ansaru ambalo lieanza harakati zake mwezi Juni mwaka jana, iliwatumia wandishi wa habari barua pepe kusema kuwa hao ndio waliohusika na kitendo hicho.
       Wizara ya mambo ya nje ya Uingereza hata hivyo ilikimya kuhusu ikiwa raia wa Uingereza alikuwa miongoni mwa wale waliotekwa nyara.
Visa vya utekaji nyara ni jambo la kawaida nchini Nigeria hasa watu matajiri na wafanyakazi wa kigeni ndio walengwa sana.

0 your comments:

Post a Comment