300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Oct 14, 2013

Tagged under: ,

Sports| Meseji za siri za Mourinho kwenye simu ya Ozil


Ukifungua simu ya Mesut Ozil utakutana na meseji za Jose Mourinho. Zipo nyingi, japo Ozil ameamua kuiweka hadharani meseji moja, inayosomeka kwa kimombo ‘Welcome to London’ kwa maana ya ‘karibu London’.
Meseji nyingine walizotumiana wawili hao ni siri yao. Ozil amesema hivyo. Haijulikani kama Mourinho anatuma meseji za aina gani kwa Ozil hasa kwa kipindi hiki anachoonyesha uwezo mkubwa wa soka katika klabu yake mpya ya Arsenal.
Kiungo huyo Mjerumani, Ozil msimu huu ameuanza kwa kasi kubwa akiwa ndani ya jezi za Arsenal baada ya kujiunga katika dakika za mwisho za siku ya kufunga usajili akitokea Real Madrid, mahali ambako alikuwa pamoja na kocha Mreno, Mourinho.
Mourinho mambo yake hayapo vizuri sana katika klabu yake ya Chelsea kwenye Ligi Kuu England na huwezi kujua nini mpango wake wa Januari mwakani baada ya mwaka huu kumkosa straika aliyekuwa akimwinda kwa nguvu zote, Wayne Rooney.
Ozil amesaini mkataba mrefu ndani ya Arsenal, lakini kwa mchezaji wa kariba yake ni lazima kikosi hicho cha Arsene Wenger kihakikishe kwamba hakitoki kapa kwenye kutwaa mataji kwa misimu isiyozidi miwili, vinginevyo kila kitu kitakuwa tofauti.
Mourinho ni kocha mwenye nguvu sana na si mtu anayemtakia mema Wenger baada ya kuzuia uhamisho wa straika Demba Ba katika dakika za mwisho, alipogundua Mfaransa huyo amemnasa kiungo mkali wa pasi fupi za mwisho, Ozil.
Jose amtumia meseji, Ozil afanya siri
Kuna kitu kinatia wasiwasi juu ya meseji wanazotumiana Mourinho na Ozil kwa sababu staa huyo wa Ujerumani anafanya siri licha ya kwamba si jambo zuri kutaka kufahamu ni kitu gani wanachozungumza wawili kwa sababu ni mambo binafsi.
Mourinho kiukweli ana wivu kwa kumwona Ozil akifanya mambo kwenye kikosi cha Arsenal, inayonolewa na kocha ambaye daima hawakuwa na uhusiano mzuri tangu awamu ile ya kwanza aliyokuwa Chelsea hadi sasa aliporejea tena kwenye klabu hiyo ya Stamford Bridge.
“Ndiyo, kuna mambo tunawasiliana. Alinitumia SMS akisema ‘karibu London’,” alisema Ozil alipozungumza na gazeti la Bild la Ujerumani.
Hata hivyo, baadaye akasema  “mengine yanatuhusu wenyewe,” wakati alipoulizwa swali ni meseji za aina gani anazotumiwa na kocha wake huyo wa zamani katika Uwanja wa Santiago Bernabeu.
Ozil amezipokea kauli za Rais wa Real Madrid, Florentino Perez kwamba asingeweza kumudu presha ya kushindania namba kwenye kikosi hicho kinachonolewa na Carlo Ancelotti kwa sasa.
Wakati mashabiki na wachezaji wenzake wa zamani katika kikosi hicho wakiwa na mapenzi makubwa na staa huyo, Ozil amekiri kuwa na bifu na klabu hiyo hasa viongozi wake.
Kuthibitisha hilo, staa huyo wa Ujerumani alisema kwa sasa amekata kabisa mawasiliano na timu hiyo na kwamba kwenye maisha yake ya soka kwa sasa Real Madrid ataishukuru kwa kumtengenezea historia na kumwezesha kucheza Ligi Kuu kubwa tatu Ulaya, baada ya kung’ara Bundesliga, La Liga na sasa Ligi Kuu England. 
Mwenyewe aichagua Arsenal
Per Mertersacker kushoto akiwa na Ozil Mazoezini

Imebainika kwamba hadi dakika za mwisho kwenye siku ya mwisho ya kufungwa kwa dirisha la usajili Ulaya, kiungo huyo alikuwa akifanya mazungumzo na klabu ya Manchester United.
Klabu hiyo inayonolewa na David Moyes ilikuwa kwenye kampeni za kumhitaji staa huyo, kabla Wenger hajatumia uzoefu wake kwa kumpigia simu Ozil na hatimaye kufanikiwa kuipata saini yake.
Baada ya kuonja benchi Real Madrid, Ozil aliamua kuchagua kwenda  Arsenal iliyochini ya Wenger mahali ambapo kuna Wajerumani wengine, Per Mertersacker na Lukas Podolski ambao inadaiwa walichangia kwa namna fulani kumshawishi kiungo huyo kutua Emirates.
Hata hivyo, kitendo cha kufuatwa na Manchester United na kufanya nao mazungumzo hadi dakika za mwisho, kisha akaichagua Arsenal ni ishara kwamba mchezaji huyo amefanya uamuzi ambao haukushawishiwa na pesa licha ya kwamba Arsenal ililipa Pauni 42.5 milioni kumnasa, huku ikimhakikishia mshahara wa nguvu.
Arsenal kupiga bao
Ozil akiwa kwenye hekaheka katika moja ya Mechi alipokuwa akiitumika Arsenal
Hadi sasa zikiwa zimechezwa mechi saba tu kwenye Ligi Kuu, Ozil ameonyesha cheche za nguvu na kuifanya Arsenal kuongoza ligi.
Kwa namna ilivyo, usajili wa Ozil utakuwa na faida kubwa muhimu kwa Arsenal kwa sababu moja, staa huyo atataka kuwaonyesha waajiri wake wa zamani, Real Madrid wanaodai kwamba mchezaji huyo hana jipya na wala hawajutii kumpoteza yeye ni mtu muhimu na kiwango chake kipo juu.

Ugomvi huo na mabosi wake wa zamani utakuwa na faida kubwa kwa Arsenal kwa kuwa wataendelea kuvuna mambo ya maana kutoka kwake anapokuwa uwanjani.
Hadi sasa Mjerumani huyo amepika mabao matano katika mechi sita za Arsenal na kuwasaidia kutamba Ligi Kuu na kuongoza pia Kundi F kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.
SOURCE:
Mwanaspot


0 your comments:

Post a Comment