300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Apr 5, 2015

Tagged under: , ,

NEWS| ACCESS BANK WATOA MSAADA KWA WATEJA WAO



Misaada iliyotolewa na Access kwa wateja wao

Benki ya Access tawi la Kahama  imeamua kusherehekea sikukuu ya Pasaka kwa kutoa msaada kwa wajasiriamali 11 toka kijiji cha Mwakata ambao pia ni wateja wao, waliokumbwa na janga la mvua ya mawe iliyouwa watu 47 na kujeruhi wengine 112.
Meneja wa Access Bank tawi la Kahama Hussein Kapilima aliyevaa tshirt nyeupe kulia kwake ni Meneja wa benki hiyo kanda ya Magharibi Prosper William katika picha ya pamoja na wateja wao
Akikabidhi msaada huo Meneja wa benki hiyo kanda ya Magharibi Prosper William amesema benki ya Access imeguswa na kilichotokea mwakata hivyo kwa kutambua umuhimu wa wateja wao wameamua kuungana kusherehekea Pasaka na wahanga hao.
Prosper amesema kushirikiana na jamii ni  moja ya wajibu wa Benki hivyo kilichowakumba watu wa Mwakata wakiwemo wateja wao kimewagusa pia na ndiyo maana wameamua kusherehekea nao Pasaka na kuahidi kuwa benki itaendelea kushiriki kwenye masuala jamii.
Jengo la Ofisi ya Access Bank tawimla Kahama
Naye Meneja wa benki hiyo tawi la Kahama Hussein Kapilima amesema benki inabidi kubadilisha mashariti ya huduma kwa wateja hao kwani hali iliyopo kwa sasa eneo la Mwakata inawawia vigumu hata wateja wao kuyamudu masharti hayo.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Mwakata Ibrahim Masanja kwa niaba ya wajsiriamali hao ameishukuru benki hiyo kwa kushiriki nao katika Pasaka na kuiomba  iendelee kuwakumbuka katika masuala mengine ikiwemo kuwapunguzia masharti katika huduma wanazozitoa.
Msaada uliotolewa na benki ya Access kwa wajasiriamali hao ambao ni wateja wa benki hiyo ni kilo 110 za Maharage,kilo 110 za Mchele,Boksi 42 za Sabuni,na Dagaa debe 22, msaada wenye thamani ya shilingi milioni 1.
Wateja wa benki ya Access toka kijiji cha Mwakata kilichokumbwa na janga la mvua iliyoambatana na upepo mkali,wakiwa katika ofisi za benki hiyo kupokea msaada

0 your comments:

Post a Comment