300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Apr 2, 2015

Tagged under: , ,

NEWS| Diamond Trust Bank (DTB) nchini yafungua tawi Wilayani Kahama

Afisa mtendaji mkuu wa Diamond Trust Bank Tanzania Limited(DTB) bi Nasim Devji akizungumza wakati wa uzinduzi wa tawi la DTB Kahama ambapo alisema hivi sasa DTB hivi sasa ina matawi 23 nchi nzima,matawi 10 yapo jijini Dar es salaam,mawili yapo jijini Arusha
 Leo Alhamis,April 2,2015 afisa mtendaji mkuu wa Diamond Trust Bank Tanzania Limited(DTB) bi Nasim Devj amezindua tawi jipya la benki hiyo lililopo katika barabara ya Ngaya/Isaka mjini Kahama mkoani Shinyanga,ambapo watu mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania wamehudhuria uzinduzi huo.Tawi la Kahama ni la tatu katika kanda ya Ziwa(mengine yapo Mwanza na Tabora) lengo likiwa ni kuhudumia jamii ya wafanyabiashara nchini Tanzania.


Mkurugenzi wa DTB Tanzania bwana Mehboob Champsi alisema akiba za wateja zimekua kwa asilimia 44.5 kutoka Tzs 399.7 bilioni mwaka 2013 hadi Tzs 577.5 bilioni,wakati mali za benki zimefikia Tzs 690.0 bilioni ikionesha ukuaji wa asilimia 36.4 kwa mwaka 2014 kutoka Tzs 505.7 bilioni kwa mwaka 2013 
 DTB inakuwa benki ya 10 ya kibiashara kufungua milango yake katika wilaya ya Kahama huki ikitoa huduma kamili za kibenki kwa watu wa Kahama

PICHA KATIKA MATUKIO KWENYE HAFLA HIYO.

Afisa mtendaji mkuu wa Diamond Trust Bank Tanzania Limited(DTB) bi Nasim Devji akimkabidhi zawadi meneja wa DTB tawi la Kahama Mercy Stephen


Afisa mtendaji mkuu wa Diamond Trust Bank Tanzania Limited(DTB) bi Nasim Devji akisaini kitabu cha wageni

Bi  Sheribanu Kurji ambaye ni mama mzazi wa
afisa mtendaji mkuu wa Diamond Trust Bank Tanzania Limited(DTB) bi Nasim Devji akikata utepe kufungua tawi la beki hiyo wilayani Kahama.






Afisa mtendaji mkuu wa Diamond Trust Bank Tanzania Limited(DTB) bi Nasim Devji akimlisha Cake meneja wa benki hiyo tawi Kahama.



Wakati wa maakuli hapa waandishi wa habari nao wakijumuika katika chakula katika hafla hiyo.







Kadama Malunde wa Malunde1 Blog naye alikuwepo akifanya yake pembeni ni Paul Kayanda wa gazeti la Mtanzania

0 your comments:

Post a Comment