hizi ni baadhi ya silaha zilizotumiwa na wavamizi nchini Nigeria |
Afsa mkuu mmoja wa jimbo hilo amefafanua kuwa lengo la mashambulizi hayo ni wizi ambapo kwa mujibu wa Gazeti la Tribune limeelezea kuwa wavamizi hao walikuwa na bunduki aina ya AK-47 na walitumia pikipiki na farasi kufanya mauaji hayo.
Kiongozi aliyeuawa alikuwa akijihami kwa kuwakataza wavamizi jambo lililopelekea kupigwa risasi mblili za kifuanai na kufa papo kwa papo.Baadhi ya waahtirika wa uvamizi huo wameelezea kuwa pengine ni kazi za kundi la upiganaji la Boko Haramu ambapo duru za kiusalama zimekanusha kundi hilo kutohusika katika mauaji hayo.
Nigeria imekuwa katika vuguvugu la masuala ya vitendo vya kigaidi vinavyotokea kwa saana maeneo ya kaskazini mwa Taifa hilo yakilihusisha kundi la Boko Haramu ikiwemo utekaji nyara na wizi.
JEE UMEIONAJE HII
ReplyDelete