300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Nov 16, 2012

Tagged under:

MICHEZO:KOCHA SERENGETI BOYS ALIA NA VIJEBA WA TIMU YA CONGO

vijana wa Serengeti Boys wakiomba kwanza kabla ya mazoezi
Kocha wa makipa wa Serengeti Boys Peter Manyika akitoa maelekezo kwa wachezaji wake katika mazoezi yaliyofanyika hii leo jioni uwanja wa Taifa
 Timu ya taifa ya Tanzania chini ya miaka 17-Serengeti Boys keshokutwa tarehe 18Novemba inajitupa katika uwanja wa taifa jijini Dar Es Salaam kupepetana na wageni timu ya tiafa ya vijana U-17 toka Congo-Brazzavile katika mchezo wa Raundim ya tatu na ya mwisho kuelekea kunako Fainali za Mataifa ya Afrika chini ya miaka 17 yanayotarajiwa kufanyika nchini Moroco mwakani.
kocha mkuu wa Serengeti Boys Jacob Michelsen akitoa maelekezo ya vitendokwa vijana wake

Serengeti Boys wamefanikiwa kufuzu raundi ya tatu kufuatia ya hasimu wake katika raundi ya kwanza na ya pili timu za Kenya na Misri ambazo zingecheza na vijana hao wa Michelsen kujitoa katika kuwania kufuzu kwa michuano hiyo.Mwaka 2005 Serengeti Boys walifanikiwa kufuzu katika michuano hiyo iliyofanyika nchini Gambia lakini hawakuweza kushiriki kufuatia shirikisho la mpira wa miguu afrika(CAF) kufungia timu hiyo kwa udanganyifu wa umri kwa mchezaji Nurdin Bakari.
Peter Manyika Peter mlinda mlango namba 1 wa Serengeti Boy
Pamoja na hayo hofu ya kupoteza mchezo huo imemwingia kocha mkuu wa Timu ya taifa ya Tanzania-Serengeti Boys Mdenmark Jacob Michelsen akiweka wazi kuwa Wakongomani hao ni wazuri na aliwatizama katika Mechi waliyocheza na Zimbabwe huku na yeye akihudhuria mechi hiyo.Michelsen amesema pamoja na wapinzani wake hao kuwa bora lakinianaamini vijana wake ambao wamefanya mazoezi mepesi leo hii katika dimba la taifa wataweza kuleta furaha kwa Watanzania kwa ushindi mzuri ikizingatiwa  kuwa vijana wake wapo katika hali nzuri kiafya wanamorali na yeye kama kocha anapata ushirikiano mzuri toka shirikisho la kandanda Tanzania-TFF.
kocha mkuu wa Serengeti Boys Jacob Michelsen  akizungumza jambo kushoto kwake ni wasaidzi wake Jamhuri Kiwhelu na Manyika Peter na upande wa kuume mwake ni makamu mwenyekiti wa kamati ya Serengeti Boys Kassim Dewji,katibu wa kamati hiyoHenry Tandau,Suleiman Nyambui na katibu mkuu TFF Angetile Osiah walipoitembelea timu hiyo wakati ikifanya mazoezi uwanja wa Taifa leo hii.

Kocha Michelsen ameongeza kuwa licha ya kuwa nyumbani mchezo huo utaenda kuwa mkali huku akiweka wazi wapinzani wake wanawachezaji waliozidi umri(vijeba) kwani katika timu hiyo ya Congo kuna baadhi ya wachezaji waliokwenda nchini Mexco kushiriki michuano ya kombe la dunia U-17 ambapo timu hiyo ilweza kutolewa kunako raundi ya pili huku akiwataja baadhi ya wachezaji ambao anawatilia shaka kuwa ni pamoja na Chaverly Mabiat na Hady Binguila.
PICHA ZAIDI  WACHEZAJI WA SERENGETI BOYS WAKIPIGA MAZOEZI .


magolikipa-Serengeti Boys wakiwajibika mazoezini




Manyika Peter baba wa Peter Manyika

0 your comments:

Post a Comment