300x250 AD TOP

Powered by Blogger.

Life & style

Popular Posts

Marafiki Waliotembelea Blog

Technology

NGOMA

Featured Video

UDAKU

Recent Posts

Popular Posts

Feb 21, 2013

Tagged under:

Sports | Kifaa Cha Umeme kuwekwa kwenye Jezi kuzuia Matatizo yanayopelekea wachezaji kupoteza Uhai kama ilivotokea kwa Vivian Foe almanusura kwa Fabrice Muamba.




            Bodi ya soka la kimataifa (IFAB) na FIFA wanajiandaa kuanza mchakato wa majaribio ya kuweka kifaa cha umeme kwenye jezi za wachezaji ili kupunguza matatizo ya kiafya kwa wachezaji yanayotokea uwanjani.Hatua hiyo itafanya vifaa hivyo kuwekwa kwenye pindo la shingo la jezi, ili kuweza kukusanya taarifa kuhusu mapigo ya moyo, joto la mwili na umbali ambao mchezaji anakuwa amekimbia uwanjani.
           Sheria za soka za sasa zinakataza mawasiliano yoyote ya kieletroniki kati ya wachezaji na makocha na watu  wanaohusika na mambo ya afya, lakini kumekuwepo na wito kuibadili sheria hiyo ili kuleta utaratibu wa kuweka vifaa vitakvyokuwa vinafuatilia maendeleo ya afya za wachezaji uwanjani, hasa kufuatiwa kutokea kwa matukio hivi karibuni ya wachezaji kama akina Fabrice Muamba, aliyendondoka uwanjani kufuatiwa kupata mshtuko wa moyo na hatimaye ikabidi aastafu soka

          Tukio hili lilishawahi kumkuta pia aliyekuwa kiungo wa kimataifa wa Cameroon Marc Vivien Foe aliyekutana na tatizo kama la Mwamba wakati timu yake ya Taifa ilipokuwa ikimenyana na Colombia katika dimba la Stade de Gerland mjini  Lyon, nchini Ufaransa ambapo dakika ya 72 kipindi cha pili na alikimbizwa Hospitalini ambapo tayari alikuwa amefariki

Marc Vivien Foe akiwa hajitambui baada ya kupoteza fahamu
Suala hili litapelekwa kwenye mkutano wa IFAB - ambayo inahusisha vyama vya soka vya England, Scotland, Wales na Northern Ireland – na FIFA katika mkutano wake wa mwaka March 3. IFAB, ambayo wanaamua sheria za mchezo, watakuwa na kura nne - moja kwa kila chama cha soka - wakati FIFA pia itakuwa itakuwa na kura nne kuamua kupitisha suala hilo.

0 your comments:

Post a Comment